Saturday, April 6, 2013

Wasichana 40 kufaidi - hazina ya Malala



Malala Yousefzai wa Pakistan
Hazina iliyoundwa na msichana wa kutoka Pakistan Malala Yousafzai imetangaza msaada wake wa kwanza katika halfa iliyoandaliwa mjini New York kwa hisani ya msanii Angelina Jolie.
Hazina hiyo ambayo iliundwa baada ya msichana huyo kupigwa risasi kichwani na kundi la Taliban mwaka uliopita itafadhili masomo ya wasichana 40 nchini Pakistan.
Akihutubia kupitia njia ya Video kutoka London Malala alisema kuwa kuvumbuliwa kwa hazina hiyo ndio siku yake ya furaha zaidi duniani.
Angelina Jolie msanii wa filamu
Bii Angelina Jolie amesema kuwa Malala mwenye umri wa miaka 15 ndiye atakayesimamia hazina hiyo na matumizi yake.
Hii itagharimu zaidi ya dola elfu arobaini na tano. Hazina hiyo ilianzishwa na Malala, kwa ushirikiano na wanaharakati wa elimu ya wasichana, mashirika yasiyo ya kiserikali na Umoja wa mataifa.
Kufikia sasa imekusanya dola nusu milioni, huku mchango mkubwa ukitoka kwa Angelina Jolie.
Hata hivyo bado ni wazi kuwa wasiwasi umetanda mjini Swat.
Hazina hiyo haijatangaza hadharani ni shule zipi zitakazofaidi na fedha hizo kwa hofu kuwa huenda zikashambuliwa na wanamgambo wa Taleban.

0 comments:

Post a Comment