FOR MORE INFORMATION ON.

ADVERTISING YOUR BUSINESS AND MARKETING !! CONTACT.+255 765 326 668

FOR MORE INFORMATION ON.

ADVERTISING YOUR BUSINESS AND MARKETING !! CONTACT.+255 765 326 668

FOR MORE INFORMATION ON.

ADVERTISING YOUR BUSINESS AND MARKETING !! CONTACT.+255 765 326 668

FOR MORE INFORMATION ON.

ADVERTISING YOUR BUSINESS AND MARKETING !! CONTACT.+255 765 326 668

FOR MORE INFORMATION ON.

ADVERTISING YOUR BUSINESS AND MARKETING !! CONTACT.+255 765 326 668

Wednesday, May 8, 2013

HATIMA YA ZOMBE NA LWAKATARE NI LEO


Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),Wilfred Lwakatare.  
MAHAKAMA ya Rufaa nchini leo inatarajia kutoa uamuzi rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Dk. Eliezer Feleshi, dhidi ya aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi, Abdallah Zombe, wa kuifuta au kutoifuta rufaa iliyokatwa na DPP baada ya jicho la mahakama kuona hati ya kukatia rufaa ina dosari.
Sambamba na hilo, pia Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, leo inatarajia kutoa uamuzi wa kuifuta au kutoifuta kesi ya tuhuma za ugaidi za kutaka kumteka mhariri wa gazeti la Mwananchi, Denis Msaki, inayomkabili Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),Wilfred Lwakatare na Ludovick Joseph.

Monday, May 6, 2013

KIINGEREZA CHAMUUMBUA DIAMOND...MASHABIKI WAMPA MAKAVU




Katika pitapita  instagram kuna picha ya msanii Diamond Platnumz alipost (hiyo hapo juu), na hapo wakatokea watu kukosoa kingereza alichotumia huku wengine wakionekana kutetea. JAMANI ENGLISH si Lugha yetu jamani. angalia hapa chini




HATIMAYE LADY JAYDEE AFUNGUKA TENA, ASEMA HATO-SURRENDER ,SOMA ALICHO ANDIKA TWEETTER


LADY JAYDEE AWAFANYA CLOUDS FM WAGOME KUPIGA NYIMBO YOYOTE YA BONGO FLEVA.....TIMES FM WASHANGILIA


 Akizungumza  katika kipindi cha Power Breakfast, Meneja wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba ameelezea kuwa Lady Jaydee  amekosea  kuelekeza  vita  kwao...


Amedai  kuwa kama tatizo ni Bendi ya SkyLight basi apambane kuipiku bendi hiyo na si kugombana na watu wengine.....

Akiongea  kwa  mbwembwe, Ruge  ameamuru  kutopugwa  wimbo  wowote  wa  bongo  fleva  leo.....

Amesema kuwa Clouds  fm ni chombo binafsi kina maamuzi ya kufanya chochote pasipo kuvunja sheria...
Baada  ya  kauli  hiyo  Times Fm  wamewajibu  clouds  fm  na  kudai  kuwa  WAO  LEO  WATAPIGA  BONGO  FLEVA  MPAKA  MAJOGOOOO...!!!   
Nadhani  Times  fm  wamefikia  uamuzi  huo  ili  kuwajulisha  clouds  kuwa  kuna  vituo  vingine  vingi vya  radio  zaidi  yao  na  kwamba  hawako  peke  yao 
Hii  ndo  tweet  yao...

"Kwa Kutumia Kilicho chetu , Asili yetu na Muziki wetu leo katika vipindi vyote utaskikia muziki wa nyumbani wa BONGO FLEVA kwa asilimia Kubwa."

PICHA ZA TUKIO ZIMA LA MLIPUKO WA BOMU KATIKA KANISA KATOLIKI HUKO ARUSHA



182591_454372931312284_641685672_n
417778_454372807978963_1620618139_n
Mmoja wa majeruhi akifikishwa hospitali 
Mmoja wa majeruhi akifikishwa hospitali
DSCN2227
Hali ya eneo mlipuko ulipotokea
DSCN2220Waumini na wananchi wengine wakiwa na shauku ya kujua kilichotokea
DSCN2228
Ulinzi umeimarishwa
DSCN2252
Viongozi wa Kanisa wakitoa taarifa ya kilichotokea kwa waandishi wa habari kabla ya Balozi wa Papa kuondolewa Kanisani hapo chini ya ulinzi mkali wa Polisi.
DSCN2246
Wanasualama Mkoa wa Arusha, wakijadiliana jambo katika eneo la tukio
DSCN2282Meya wa Manispaa ya Arusha, Mh gaundence Lyimo akielekea eneo la tukio kwa miguu baada ya utaratibu wa kutumia magari kuwa mgumu kutokana na idadi kubwa ya watu na magari yaliyoziba njia.
DSCN2258
Magesa Mulongo akiteta na RCO wa Mkoa wa Arusha
DSCN2273
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, magesa Mulongo akijiandaa kuzungumza na wananchi kanisani hapo na kuahidi kuwa Serikali itahakikisha watu wote waliohusika na jaribio hilo ovu, pamoja na mtandao wao wanakamatwa. Alidai pia vikosi vya Jeshi maalumu kwa kuchunguza milipuko vitafika eneo hilo ili kufanya uchunguzi. Taarifa za eneo la tukio zinaeleza kuwa tayari kuna mshukiwa mmoja ameshatiwa mbaroni na yuko mikononi mwa Jeshi la Polisi kwa mahojiano na uchunguzi zaidi.
DSCN2236
Eneo lenye utepe ndipo kitu hicho kinachodhaniwa kuwa bomu kilipoangukia. Pichani unaweza kuona wigi za kichwani na viatu vya waumini vikiwa vimesambaa baada ya wenyewe kuviacha, miongoni mwao wakiwa ni majeruhi.
DSCN2251
DSCN2267
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo akizungumza na mmoja wa mapadri wa Kanisa hilo kupewa maelezo ya kuhusu kilichotokea kanisani hapo.
DSCN2276
DSCN2255
DSCN2281
DSCN2225
DSCN2222
DSCN2215
DSCN2218
DSCN2219
(2746)

BREAKING NEWS: KANISA KATOLIKI LALIPULIWA NA BOMU JIJINI ARUSHA WAKATI MISA IKIENDELEA


Arusha_Clocktower
Kanisa katoliki parokia  ya Olasiti ambalo leo hii lilikuwa linapandishwa hadhi na kuwa Parokia limelipuliwa na  kitu  kinachosemekana  kuwa  ni  bomu, watu wengi wamejeruhiwa  na  mtu  mmoja  inasemekana  amefariki  dunia…. ….
Tukio  hilo  limetokea  wakati  Misa ikiwa ndio inaanza .Ilikuwa ni saa 5 kamili…Kabla Askofu hajaanzisha sala , mlipuko mkubwa  ulitokea  ndani  ya  kanisa  hilo……Mgeni rasmi   katika  hafla  hiyo  alikuwa  ni   balozi wa Vatican nchini Tanzania. … Habari zaidi   zinakuja

Saturday, May 4, 2013

Serikali yachukua uamuzi mgumu, yafuta matokeo


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, akiwasilisha kauli ya serikali Bungeni Dodoma jana kuhusu taarifa ya awali ya Tume ya Taifa ya kuchunguza matokeo ya mtihani wa taifa wa Kidato cha nne wa mwaka 2012. Picha na Edwin Mjwahuzi 
Dodoma/Dar. Serikali imechukua uamuzi mgumu na kuamua kuwafariji wanafunzi waliofeli mitihani ya kuhitimu kidato cha nne mwaka 2012 baada ya kufuta matokeo hayo na kuamua yaandaliwe upya kwa kutumia utaratibu uliotumika mwaka 2011.
Uamuzi huo wa Serikali umetokana na matokeo mabaya ya mitihani huo yaliyosababisha zaidi ya asilimia 60 ya wanafunzi kupata sifuri.
Kutokana na matokeo hayo, Serikali iliunda Tume inayoongozwa na Profesa Sifuni Mchome kuchunguza matokeo hayo ili kupata ufumbuzi wa kudumu.
Muda mfupi baada ya tamko la Serikali, baadhi ya wadau wa elimu wameeleza kufurahishwa na uamuzi huo, huku Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kikiikosoa hatua hiyo, kuwa imekiuka sheria na kupora madaraka ya Baraza la Mitihani Tanzania (Necta).
Akitoa kauli ya Serikali bungeni kuhusu taarifa ya awali ya Tume ya Taifa ya Kuchunguza Matokeo ya Mtihani wa Taifa Kidato cha nne mwaka 2012 jana, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uratibu na Bunge), William Lukuvi alisema wameagiza Necta kuweka viwango ili matokeo ya wanafunzi yalingane na juhudi zao.
“Standardization ifanyike ili matokeo ya wanafunzi yalingane na juhudi wazizoziweka katika kusoma kwa mazingira, hali halisi ya Tanzania na uamuzi wa taifa kuongeza idadi ya shule na wanafunzi wakati uwekezaji katika ubora unaendelea,” alisema Lukuvi.
Lukuvi alisema Necta imeelekezwa kuwa licha ya sheria ya kuanzishwa kwake kuruhusu kufanya marekebisho ya mchakato wa mtihani, marekebisho yoyote ya kubadilisha utaratibu wa kupanga viwango vya ufaulu na madaraja ya mitihani yanatakiwa yahusishe wadau wote wanaohusika na mitalaa, ufundishaji na mtihani.
“Wakati Tume inaendelea kukamilisha kazi yake, uamuzi wa Necta kutumia utaratibu mpya wa kupanga viwango vya ufaulu na madaraja ya matokeo ya mitihani uliotumika 2012 usitishwe,” alisema Lukuvi na kuongeza:
“Badala yake Necta itumie utaratibu uliotumika mwaka 2011 kwa kidato cha nne na sita kwa mitihani yote, ikiwamo utaratibu wa Standardization na kutoa matokeo mapya kwa kuzingatia maelekezo haya.”
Pia, Serikalli imeagiza mchakato wa tuzo wa taifa (National Qualifications Framework) na Mfumo wa Kutahiniwa/ kuthamini maendeleo ya mwanafunzi masomo yake (National Assessment Framework) ukamilishwe haraka iwezekanavyo.
Katika mtihani wa mwaka 2012, wanafunzi 367,756 walifanya mtihani huo na waliofaulu ni 126,847. Waliofaulu kwa kwa madaraja ya kwanza hadi la tatu ni 23,520 sawa na asilimia 6.4 na daraja la nne ni 103,327 sawa na asilimia 28.1, huku 240,909 ambao ni asilimia 65.5 wakipata daraja sifuri.
Kauli ya CWT
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Ezekiel Oluoch alisema Baraza la Mawaziri limepora kazi za Bodi ya Baraza la Mitihani kwani ndio yenye jukumu la kufuta matokeo kisheria.
Mbali na hilo Oluoch alisema bado wanafanya utafiti ili kuona kama Baraza la Mawaziri lina uwezo wa kufuta matokeo na kuamuru mitihani isahihishwe upya, badala ya Bodi ya Baraza la Mitihani.
Oluoch aliyesema tamko rasmi la CWT kuhusu uamuzi huo wa Serikali litatolewa wiki ijayo, alieleza kuwa kwa sasa wanachunguza kuona kama jambo hilo lina usahihi kwa kiasi gani.
“Mitihani iliyofutwa ilitolewa na Bodi ya Necta ambayo ndio itakuwa na jukumu la kusimamia usahihishaji mpya na kutangaza tena matokeo.
Kama hali yenyewe ndio hiyo ni wazi kuwa haina tena uwezo wa kusimamia jambo hilo, inatakiwa kung’oka na kuundwa bodi mpya,” alisema Oluoch na kuongeza;
“Nasema hivyo kwa sababu hawawezi kula matapishi yao kwa kuwa wao ndio wenye mamlaka ya kutoa tena matokeo hayo na walishasema kuwa yalikuwa mabaya, sasa uzuri wake utatoka wapi tena.”
Alisema kuwa kufutwa kwa matokeo hayo kunaonesha wazi kuwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imeshindwa kazi ya kusimamia elimu nchini.
“Pia katika utangazaji wa matokeo anatakiwa waziri mpya wa kufanya hivyo kwa kuwa huyu wa sasa alieleza sababu za wanafunzi kufeli, sasa akiwa anatangaza matokeo mapya atatueleza nini,” alihoji.
Sababu za matokeo mabaya
Waziri Lukuvi alisema takwimu zinaonyesha kushuka kwa ufaulu huo unahusu shule zote na asilimia kwenye mabano, shule za wananchi (1.82); Shule za umma yaani kongwe (6.43); Binafsi (6.39) na Seminari (7.29).
Kuhusu matokeo ya kidato cha nne 2012, Lukuvi alisema tume imebaini licha ya wanafunzi kuwa kwenye mazingira yanayofanana na wenzao waliopita, ufanisi umekuwa ukishuka kwa sababu mbalimbali.
“Ufaulu wao umeshuka zaidi kwa sababu ya mabadiliko ya mchakato wa kuandaa na kutoa matokeo ya mtihani mwaka 2012, mfumo uliotumika kupanga matokeo na madaraja ni tofauti na ule uliotumika miaka iliyotangulia,” alisema Lukuvi na kuongeza:
“Uchunguzi unaonyesha kuwa mwaka 2011, Necta lilikuwa linachakata alama za mwisho kwa kutumia mfumo ambao ulikuwa unabadilika kutegemea hali ya ufaulu kwa mwanafunzi ambao ni National Mean Difference (NMD).
Alisema uataribu huo ulitokana na tofauti ya wastani wa kitaifa wa alama za maendeleo, kutoka alama ya maendeleo endelevu (Continued Assessment-CA) za watahiniwa wote na wastani wa kitaifa wa ufaulu wa mtihani wa mwisho kwa somo husika.
Aliendelea kuwa kila mtahiniwa aliongezewa NMD iliyokokotolewa kwenye alama za mtihani wa mwisho, ili kupata alama itakayotumika kupada daraja la ufaulu.
“Lakini mwaka 2012 lilitumia mfumo mpya wa kuwa na viwango maalumu vya kutunuku (Fixed Grade Range). Tume imebaini kwamba licha ya mfumo huo ulioandaliwa kwa nia nzuri, utaratibu huo mpya hakufanyiwa utafiti wa maandalizi ya kutosha kabla ya kutumika,” alisema.
Lukuvi alisema taarifa ya awali ya tume, inaonyesha kutokana na uchunguzi uliofanyika kwa muhtasari imebaini mambo mbalimbali.
Alisema matokeo ya  kidato cha nne kuanzia mwaka 2008 yamekuwa na mserereko wa kushuka tofauti na miaka iliyotangulia, kwa sababu ya changamoto zinazotokana na mafanikio yaliyopo sasa ya kuongezeka kwa idadi ya shule za msingi na sekondari, hususan mwaka 2011 na 2013 hivyo kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi.
“Mwaka 1961 hadi 2011 idadi ya wanafunzi kwa shule za msingi imeongezeka kutoka 486,470 hadi 4,875,764, sawa na ongezeko la wanafunzi 4,389,294 kwa takriban miaka 40,” alisema.
Alisema wanafunzi wameongezeka kutoka 4,875,764 mwaka 2001 hadi 8,247,472 mwaka 2012, sawa na ongezeko la wanafunzi 3,371,708 kwa kipindi cha miaka 11.
Sekondari wanafunzi wameongezeka kutoka 11,832 mwaka 1961 hadi 289,699 mwaka 2001 sawa na ongezeko la wanafunzi 274,867 kwa miaka 40.
Lukuvi alisema kati ya mwaka 2001 hadi 2012 wanafunzi wameongezeka kutoka 289,699 hadi 1,884,270 sawa na ongezeko la watu 1,594,571.
Tume hiyo imebaini changamoto nyingine ni mazingira yasiyo ya kuridhisha ya kufundishia na kujifunzia, ikiwamo upungufu wa miundombinu muhimu ya shule; madarasa, madawati, maktaba, nyumba za walimu, bweni na majengo mengine muhimu.
“Kuna tatizo la uhaba wa walimu, vitabu, zana za kufundishia na matatizo ya ukaguzi wa shule. Vilevile tumebaini Mfumo wa Elimu ya Msingi na Sekondari unakabiliwa na changamoto nyingine mbalimbali ambazo taifa linapitia kwa sasa,” alisema Lukuvi na kuongeza:
“Yapo masuala ya sera, sheria, mfumo, muundo na changamoto za uhaba wa rasilimali fedha na watu. Tume inaendelea kufanyia kazi maeneo haya kwa kushirikiana na wataalamu na wadau wengine.”

source: Mwananchi

AJALI YAUA ZAIDI 5 WENGINE ZAIDI YA 20 WAJERUHIWA VIBAYA IRINGA JANA JIONI



 Moja kati ya ajali ya basi la Taqwa (picha na maktaba yetu)
.......................................................

Abiria zaidi watano waliokuwa wakisafiri na basi la kampuni ya Taqwa lenye namba za usajili T 273 CDR kutoka jijini Dar es Salaam kwenda Malawi wamekufa papo hapo na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa vibaya katika ajali iliyotokea jioni hii katika eneo la Nyololo wilaya ya Mufindi mkoani Iringa.

Akizungumza na mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com mmoja kati ya mashuhuda aliyejitambulisha kwa jina la Dkt Matatala alisema kuwa ajali hiyo imetokea mida ya saa 11 jioni wakati basi hilo likitokea Dar es Salaam kwenda nchini Malawi.

Alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni lori lenye namba za usajili T 104 DZZ ambalo lilikuwa likitokea Makambako kuelekea Iringa,lori lililokuwa likijaribu kulipita lori lenye namba za usajili T 227 AVC na kushindwa kupita na kuishia kugongana uso kwa uso na basi hilo ambalo pia lilikuwa likija kwa mwendo wa kasi.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo wamesema kuwa ajali hiyo imetokea katikati ya mji wa Nyololo ambapo ni jirani kabisa na eneo lenye matuta ya kuzuia magari kwenda kwa mwendo kasi.

 Alisema kuwa hadi majira ya saa 12.45 jioni maiti tano zilikuwa zimetolewa katika basi hilo la Taqwa na kuwa jitihada za wasamaria wema kutoa maiti na majeruhi katika eneo hilo zimeendelea kufanyika.

Mbali ya maiti hizo pia alisema jumla ya majeruhi 20 waliokolewa na kukimbizwa katika Hospitali ya wilaya ya Mufindi kwa matibabu zaidi. Dkt Matatala alisema kuwa katika tukio hilo wananchi wameweza kuimarisha ulinzi zaidi katika eneo hilo ikiwa ni pamoja na kulinda mali za majeruhi na abiria waliopoteza maisha yao kwa ajili hiyo.

Wakati huo huo wananchi wa eneo hilo la Nyololo wameelekeza lawama zao kwa jeshi la polisi wilayani Mufindi kwa kuchelewa kufika katika eneo la tukio na kuwa taarifa wamepewa mapema ila hadi majira ya saa 12.50 hakukuwepo na askari aliyefika eneo hilo.

Hii ni ajali ya pili kutokea katika wilaya ya Mufindi kwa kipindi cha wiki moja baada ya ajali nyingine mbaya kama hii kutokea eneo la Mafinga kwa gari ndogo iliyokuwa ikiendeshwa na paroko wa kanisa katoliki Ifunda marehemu Alfonce Mhamilawa kutokea kwa kuingia nyuma ya lori. 
CHANZO; http://www.matukiodaima.com/

Wenger - Relegated QPR will be a threat


Arsène Wenger
Arsène Wenger
Arsène Wenger refuses to discount the threat of Queens Park Rangers in Saturday’s London derby.
Harry Redknapp’s team were relegated along with Reading after drawing 0-0 at the Madejski Stadium last Sunday.

But Manchester City, Chelsea and Tottenham all failed to win at Loftus Road this season and Wenger says players will need to be at their best to take three points.
“In the Premier League, we watched their recent three or four games,” said Wenger. “All the games were tight, so we want to make sure that this little percentage goes for us. [We need] more focus, more determination.
“It can happen yes, that they play under less pressure, with less fear. It can be of course very dangerous.
“I still believe that the derby will be decided by the quality of our performance. If we continue to play like we do, we will make it and that’s what we focus on.”

MWANAFUNZI WA CHUO CHA IFM -DAR AFARIKI DUNIA KWA KULISHWA SUMU NA MKE WA MTU



Habari   zilizotufikia  toka  IFM- Dar es salaam  ni  kwamba  mwanafunzi  mmoja ambaye  bado  hatujafanikiwa  kulipata  jina  lake  amefariki  dunia  kwa  kulishwa  sumu  katika  chakula  alicholetewa  na  mpenzi  wake  ambaye  ni  mke  wa  mtu......

Taarifa  zaidi  zinadai  kwamba Mwanafunzi huyo alikuwa na uhusiano wa karibu sana na mke  wa mtu  ambaye  mbali  na  starehe  za  kimapenzi  alikuwa  pia  anampekea  chakula  cha  jioni


Baada ya  mchezo  huo  kudumu  kwa  muda, mume wa  mwanamke  aliusoma  mchezo  mzima  na  kuandaa  tego  la  kuwaangamiza  wote....

Habari  zinadai  kwamba  Siku ya jumatano jioni mwanaume  huyo aliwahi  kurudi  nyumbani   na  kufanikiwa  kukinasa  chakula  kilichokuwa  kimeandaliwa  tayari  kwa  kupelekwa  kwa  huyo  mwanafunzi  ambaye  alikuwa  anatembea  na  mke wake.....

Baada  ya  kukinasa, alijifanya  kuzuga  na  kupotezea...Mkewe  alipotoka  alikichukua  na  kukitia  sumu  chakula  hicho  na  kisha  kukiweka   kama  kilivyokuwa  kimeandaliwa....

Lengo  lake  lilikuwa   ni  kuwamaliza  wote  maana  alijua  ni  lazima  akifika  watakaa na kula  pamoja.....

Mwanamke alipopeleka chakula  hakukaa  kula  na  badala  yake   alimwambia yule mwanafunzi   kuwa  mume wake amewahi kurudi siku  hiyo  hivyo  hatoweza  kukaa  wale  pamoja....Mwanafunzi  huyo  akakipokea  na  kukila  na  ndipo  mauti  yakamkuta 


Habari  toka  chuoni  hapo  zinadai  kwamba  mwanafunzi  huyo  alikuwa  ameshadisco  lakini  alikuwa  amepewa  nafasi  nyingine  ya  kurudia  mwaka  wa  pili , hivyo aliendelea kukaa mtaani kama mwanafunzi....


Mwili wa marehemu bado uko Muhimbili kwa uchunguzi zaidi baada ya polisi kuuzuia kuzikwa....

Hizi  ni  habari  mbaya  sana  kwa  wanafunzi  wa  chuo  hicho maana ni jumatatu  tu  mwanafunzi mwingine  alifariki  katika  hali  ya  kutatanisha baada ya  kifo cha mpenzi  wake   miezi  michache  iliyopita....

Habari za ndani zaidi zinadai   kuwa toka  mwaka  huu  uanze  mpaka sasa chuo  cha IFM  kimepoteza wanafunzi 12 huku  wawili  wakiripotiwa  kuwa  na  hali  mbaya  zaidi  katika  hospitali  ya Muhimbili....



Mtandao  huu  unaendelea  kuifuatilia  habari  hii  kwa  kina  zaidi

HILI NDILO KANISA HUKO UINGEREZA AMBALO WAMEAMUA KUSHARE NA WAISLAMU. CHEKI PICHA NA STORY HAPA

 

church uk muslims worshippers prayers
A Scottish church has become the first in the UK to share its premises with Muslim worshippers.
According to Daily Mail, St John’s Episcopal Church in Aberdeen now welcomes hundreds of Muslims praying five times a day in their building as the nearby mosque was so small that they were forced to worship outside.
The minister of St John’s, Rev Isaac Poobalan, has handed over part of the church hall to Chief Imam Ahmed Megharbi and the imam has led prayers in the main chapel.
Rev Poobalan said today that he would not be true to his faith if he did not offer to help.
Rev Poobalan, 50, said being surrounded by Islam while growing up in India helped break down the divide for worshippers of two religions praying together in Aberdeen.
Sheikh Ahmed Megharbi of the Syed Shah Mustafa Jame Masjid mosque said: ‘What happens here is special and there should be no problem repeating this across the country.
‘The relationship is friendly and respectful.’
St John’s is part of the Scottish Episcopal Church, which is part of the Anglican Communion and distinct from the presbyterian Church of Scotland.
The relationship between the mosque and St John’s has developed over the past few years.
On Christmas Eve 2010 both opened their doors for prayers, food and socialising.
In 2011, the church and mosque teamed up to mark the 10th anniversary of the 9/11 terrorist attacks in the USA.
Verses were read from both the Bible and the Koran to commemorate those who died.
There have been cases of Christians allowing Muslims to pray in their churches in parts of America.
In 2011, two Florida churches were criticised for opening their doors to Muslim groups.
But Church leaders believe the move in Aberdeen is a first for the United Kingdom.

JB ATANGAZA ATAKAPOGOMBEA UBUNGE MWAKA 2015, SOMA ALICHOKISEMA HAPA


HATIMAYE nguli wa sanaa za maigizo Bongo, Jacob Stephen Mbura ‘JB’ amelianika jimbo atakalogombea ubunge mwaka 2015.

JB aliyaongea hayo mwanzoni mwa wiki hii, jijini Dar es Salaam ambapo alisema macho yake yote yapo 


Mkoa wa Dar es Salaam ambao una majimbo nane.

JB: Niliposema natangaza kugombea ubunge mwaka 2015 wengi waliamini ni maneno tu, lakini nia yangu ni sahihi. Nitagombea na leo nasema jimbo langu lipo Mkoa wa Dar es Salaam.


Aliongeza kuwa, jimbo atakalogombea litaendelea kubaki kuwa siri ya moyo wake na meneja wake wa kampeni ambaye hakupenda kumtaja jina.


Majimbo yanaounda mkoa wa Dar es Salaam katika uwakilishi bungeni ni Ukonga, Ilala, Kinondoni, Segerea, Kawe, Kigamboni, Ubungo na Temeke.

mourinho kurudi tena chelsea

Mourinho arudi rasmi Chelsea



Kocha Jose Mourinho
LONDON, ENGLAND
HATIMAYE kocha, Jose Mourinho, amekubali kuinoa tena Chelsea kwa mkataba mnono wa pauni 10 milioni na kumekuwa na taarifa kwamba atatua rasmi Stamford Bridge, Julai Mosi.

Habari zinasema kocha huyo wa Real Madrid alikutana na mmiliki wa Chelsea, Roman Abramovich na kupata chakula cha usiku kwenye mgahawa wa La Famiglia jijini London ambapo walifanya mazungumzo ya kina na kocha huyo alikubali kutua Chelsea kwa dau hilo.

Hata hivyo kocha huyo atatakiwa kuweka mambo sawa kati yake na uongozi wa Real Madrid kwa kuwa bado ana mkataba kwenye klabu hiyo unaomalizika baada ya miaka mitatu.

Habari zinasema Abramovich atatakiwa kutoa kiasi cha pauni 12 milioni kwa Real Madrid ikiwa ni gharama ya kuvunja makataba wa kocha huyo.

Chelsea itamtambulisha kocha huyo kabla ya kuanza kwa ziara za mechi za kirafiki, hiyo inamaanisha kuwa mechi ya kwanza ya kocha huyo itakuwa dhidi ya Singha All Stars XI huko Thailand, Julai 17.

Msaidizi wa zamani wa Mourinho, Andre Villas-Boas, alisema anaamini kocha huyo ameshasaini mkataba mpya.

Kocha huyo wa Tottenham, ambaye aliwahi kufanya kazi kwenye klabu alizopitia Mourinho, Porto na Chelsea alisema: "Nina uhakika uamuzi wa mwisho umeshafanyika. Nadhani anafurahi kurudi England, ni kama nyumbani kwake.

"Huwa si jambo la kawaida kuona mtu akisema ataondoka kwenye klabu fulani wakati hajakamilisha mipango."

Villas-Boas aliongeza: "Ana historia nzuri kwenye ligi hii, nadhani atatoa changamoto baada ya kuwasili hapa. Wachezaji wanampenda na wamekuwa wakitaja jina lake mara kwa mara."

Akiwa Chelsea, Mourinho alipata ubingwa wa Ligi Kuu England msimu wa 2004/2005 na 2005/2006 pia alipata Kombe la FA msimu wa 2006/2007.

Alipata vikombe vya ligi msimu wa 2004/2005, 2006/2007 na Ngao ya Hisani, 2005.

LISSU: CCM IMEINGILIA MCHAKATO WA KATIBA.

ADAI FEDHA ZILIZOOMBWA KWA AJILI YA TUME NI KUFURU.http://www.freemedia.co.tzMbunge wa Singida Mashariki na Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu.
 
MSEMAJI Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa Wizara ya Katiba na Sheria, Tundu Lissu amedai kuwa matumizi ya fedha zilizoombwa kwa ajili ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ni kufuru.

Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki kwa tiketi ya CHADEMA, alitoa kauli hiyo wakati akitoa maoni ya kambi ya upinzani kwa bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa mwaka ujao wa fedha 2013/2014.

Alisema katika mwaka wa fedha 2013/14, Bunge linaombwa kuidhinisha sh bilioni 33.944, sawa na kiasi kile kile kilichoidhinishwa mwaka wa fedha uliopita.

Lissu alisema kiasi hicho ni pamoja na sh bilioni 12.193 kwa ajili ya kulipia posho za vikao kwa wajumbe wa tume 34 na sekretarieti 160, sh bilioni 1.728 kwa ajili ya posho ya kujikimu kwa wajumbe na sekretarieti wanaposafiri nda
ni ya nchi kikazi na sh bilioni 1.650 kwa ajili ya kulipa gharama za nyumba za wajumbe na sekretarieti wanaotoka nje ya Dar es Salaam.

Akichanganua matumizi ya tume hiyo, inayoongozwa na Jaji Joseph Warioba, Lissu alisema kuna sh milioni 18 zinazoombwa kwa ajili ya kugharamia chakula kwa wajumbe wa tume na sekretarieti watakaopata maambukizi ya ukimwi.

“Kambi rasmi ya upinzani bungeni inaitaka Serikali ya CCM itoe kauli rasmi mbele ya Bunge lako tukufu kama kuna uhalali wowote wa kutumia fedha za wananchi ili kununua ‘chakula maalumu’ kwa ajili ya wajumbe na sekretarieti ya tume watakaopata ukimwi kwa sababu ya kuendekeza ngono zembe na starehe zao binafsi,” alisema.

Lissu alisema wajumbe hao ambao wengi ni wazee, wanatakiwa wafanye kazi ya tume vinginevyo Bunge lielezwe kwa ufasaha ni kwa namna gani mchakato huu wa Katiba mpya unatazamiwa kusababisha maambukizi ya ukimwi kwa wajumbe hao.

Kwa mujibu wa Lissu, pia kuna sh milioni 60 kwa ajili ya usafiri wa ndani, sh milioni 50 kwa ajili ya gharama za malazi kwa wajumbe wa tume na sekretarieti wanaposafiri kikazi, sh milioni 423 kwa ajili ya chai na vitafunwa na sh milioni 50 kwa ajili ya wahudumu wanaosaidia kazi za tume wakiwa mikoani wakati wa kushiriki kwenye mabaraza ya katiba na shughuli za upigaji kura ya maoni.

Lissu alisema vile vile, Bunge limeombwa kuidhinisha sh milioni 60 ya kulipia maji kwa matumizi ya ofisi za tume, sh milioni 30 kwa ajili ya kulipia gharama za usafiri wa basi na teksi kwa wajumbe na sekretarieti watakaposafiri ndani ya nchi kikazi na sh milioni 103 kwa ajili ya kulipia gharama za simu za mkononi.

Akiendelea kuanika matumizi ya tume hiyo, Lissu alisema Bunge linaombwa kuidhinisha posho na ulaji zaidi ya huu kwa ajili ya wajumbe na sekretarieti ya tume.

Alisema ulaji huu mwingine unajumuisha sh milioni 604 kwa ajili ya posho kwa wajumbe wa tume na sekretarieti wakati wa Bunge Maalumu la Katiba.

Alisema maelezo ya tume yamejaribu kuhalalisha matumizi ya fedha hizi za ziada kwa kuzibatiza jina la ‘posho ya mazingira magumu’, wakati vikao vya Bunge Maalumu la Katiba vitafanyika jijini Dar es Salaam au Dodoma.

Lissu aliongeza kuwa zipo sh milioni 266 zinazoombwa kwa ajili ya chakula na viburudisho wakati wa vikao vya Bunge Maalumu la Katiba, sh milioni 12 nyingine kwa ajili ya huduma za chakula na viburudisho kwa shughuli zinazohusiana na tume na sh milioni 185 kwa ajili ya kulipia usafiri wa basi na teksi.

Aidha, alisema kuna sh milioni 30 za utengenezaji wa fulana na kofia kwa wajumbe wa tume na sekretarieti wakati wa kushiriki kwenye uhamasishaji kuelekea upigaji wa kura ya maoni, sh milioni 40 nyingine kwa ajili ya utengenezaji wa sare wakati wa maadhimisho mbalimbali ya kitaifa na sh milioni 12 kwa ajili ya posho za kujikimu kwa watumishi wa tume watakaohudhuria kwenye maadhimisho mbalimbali ya kitaifa.

“Kwa ujumla, Mheshimiwa Spika, Bunge lako tukufu linaombwa kuidhinisha jumla ya sh bilioni 19.039 kwa ajili ya posho za aina mbalimbali na malipo mengine yanayowahusu wajumbe na sekretarieti ya tume kwa mwaka wa fedha 2013/14. 

Hii ni zaidi ya asilimia 56 ya bajeti yote inayoombwa kwa ajili ya tume,” alisema.

Kwa mahesabu hayo, Lissu alisema wajumbe wa tume, katibu na naibu katibu pamoja na wakuu wa vitengo saba vya tume na madereva wao, kila mmoja atalipwa wastani wa sh milioni 16.756 kwa mwezi huo mmoja, au sh 558,547 kama posho ya kujikimu kwa kila siku moja.

“Mheshimiwa Spika, katika nchi ambayo wauguzi katika hospitali za umma wanalipwa mshahara wa kuanzia takriban sh 360,000 kwa mwezi na walimu wa shule za msingi wanaanzia sh 250,000 na wale wa sekondari sh 325,000 kwa mwezi, malipo haya kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba yana uvundo na harufu mbaya ya rushwa kwa wajumbe wa tume,” alisema Lissu.

Mabaraza ya Katiba.
Lissu alisema Februari mwaka huu, tume ilichapisha mwongozo kuhusu muundo, utaratibu wa kuwapata wajumbe wa mabaraza ya katiba ya wilaya (Mamlaka za Serikali za Mitaa) na uendeshaji wake.

Alisema mwongozo huo ulisainiwa na Mwenyekiti wa Tume Jaji Warioba na ulianza kutumika Machi Mosi, mwaka huu.

Alisema ingawa tume imedai kwamba mwongozo huo ulitolewa kwa kuzingatia matakwa ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, kambi hiyo inaamini kwamba ulitolewa kinyume na matakwa ya sheria hiyo na kwa lengo la kuinufaisha CCM na washirika wake.

Kwa maana hiyo, alisema mikutano ya uchaguzi wa mabaraza ya katiba ya wilaya kwa upande wa Tanzania Bara imeendeshwa na makada wa CCM wakati kwa upande wa Zanzibar imeendeshwa na viongozi waliochaguliwa na wananchi walioshiriki katika mikutano hiyo bila kujali itikadi au uanachama wao katika vyama vya siasa.

Alisema ndiyo maana karibu nchi nzima wananchi wengi wasiokuwa wanachama wa CCM ambao walipata kura nyingi katika kura za mikutano ya uchaguzi ya vijiji na mitaa walienguliwa kwenye michujo iliyofanyika katika kamati za maendeleo za kata zilizowekwa kwa mujibu wa mwongozo wa tume.

Lissu alisema hata mahali ambapo wananchi wasiokuwa wanaCCM walifanikiwa kupenyeza katika chekeche la kamati za maendeleo za kata (WDC) wamefanyiwa mizengwe na wanaCCM ili waondolewe katika orodha ya wajumbe wa mabaraza ya katiba ya wilaya.

Alisema mfano mzuri ni Beatus Kipeya aliyechaguliwa mjumbe wa Baraza la Katiba la Wilaya ya Arusha Mjini kwa kupitia Kata ya Sombetini.

Alisema mara baada ya Kipeya kuchaguliwa kwenye kikao cha Kamati ya Maendeleo ya Kata ya Sombetini cha tarehe 8 Aprili, 2013, siku hiyo hiyo Katibu wa CCM Wilaya ya Arusha, Allan G. Kingazi alimwandikia Mkuu wa Wilaya ya Arusha kumlalamikia juu ya kuchaguliwa kwake.

Alisema ukiacha Ofisa Uhamiaji wa Mkoa wa Arusha, watu wengine wote walionakiliwa barua ya malalamiko ya Katibu wa CCM Kingazi ni makada wa CCM.

“Wote hawa hawahusiki kisheria kwa namna yoyote ile katika mchakato wa uundaji wa mabaraza ya katiba ya wilaya. Chombo pekee ambacho kinahusika kisheria na mchakato wa kuunda mabaraza hayo na ambacho kilitoa mwongozo wa namna ya kuyaunda, yaani tume, haikuandikiwa wala kunakiliwa barua ya malalamiko ya Katibu wa CCM Kingazi,” alisema.

Lissu aliongeza kuwa endapo serikali itashindwa kutekeleza ahadi ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati akihitimisha mjadala wa bajeti ya ofisi yake, na endapo muswada utakaoletwa hautakidhi matakwa ya kuboresha mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya, basi CHADEMA itahamasisha Watanzania kuikataa rasimu ya katiba mpya kwenye kura ya maoni.

“CHADEMA itawaalika wanachama, wafuasi na mashabiki wake Tanzania nzima, pamoja na taasisi za kiraia na za kidini, vyama vya siasa na Watanzania wote wenye nia njema na taifa hili kuhamasisha Watanzania kuikataa rasimu ya katiba mpya kwenye kura ya maoni,” alisema.

Friday, May 3, 2013

AIBU: MREMBO ATUPWA JELA MIEZI 6 BAADA YA KUNASWA AKIJIUZA.....MCHUMBA WAKE AMWAGA MACHOZI HADHARANI


MREMBO Brandina Barthon (24), Jumatatu iliyopita alihukumiwa kwenda jela miezi 6 baada ya kupatikana na hatia kwenye kesi ya ukahaba iliyokuwa ikimkabili katika Mahakama ya Sokoine Drive (Jiji) jijini Dar.

Brandina alisomewa hukumu hiyo na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, William Mutaki ambaye alisema kutokana na ushahidi uliothibitika, mahakama hiyo inamhukumu kwenda jela miezi 6, ili liwe fundisho kwa wengine.

Hukumu hiyo ilimfanya mrembo huyo kuchanganyikiwa na kuangua kilio lakini mheshimiwa hakimu aliamua kukazia hukumu yake bila ya kupepesa macho.
 
Wakati mwanamke huyo akiangua kilio, afande wa Jeshi la Magereza alimfikia na kumchukua  kwa ajili ya kumpeleka kwenye Karandinga kuelekea Gereza la Segerea kuanza maisha ya jela.

Mbali na Brandina, mwanaume aliyedaiwa kuwa ni mpenzi wa mtuhumiwa huyo aliyekuwa akifuatilia kesi hiyo naye alimwaga machozi baada ya kutolewa hukumu hiyo.

Thursday, May 2, 2013

Mume mwenye wake 39, watoto 94




1 man (Ziona Chana, Indian), 39 wives, 94 children, 14-daughters-in-law & 33 grandchildren.

He is head of the world’s biggest family – and says he is ‘blessed’  to have his 39 wives.

Ziona Chana also has 94 children, 14-daughters-in-law and 33 grandchildren.


They live in a 100-room, four storey house set amidst the hills of Baktwang village in the Indian state of Mizoram, where the wives sleep in giant communal dormitories.

You treat this place like a hotel: With 100 rooms the Ziona 
mansion is the biggest concrete structure in the hilly village of 
Baktawng
The wives and I: Mr Ziona Chana poses with his 39 wives at 
their home in Baktawang, Mizoram, India
Shared bedroom: A look inside the four-storey mansion, 
Chhuanthar Run - The House of the New Generation