Tuesday, April 2, 2013

TAHADHARI YA VITA, PAPA AOMBA AMANI KOREA


Papa Francis akizungumza na umati wa watu katika uwanja wa Mtakatifu Peter  jijini Vatican, kwenye salamu zake 'kwa jiji na ulimwengu.' "Urbi et Orbi". © Reuters/Stefano Rellandini
Salamu za mara ya kwanza kutoka kibaraza cha Mtakatifu Basilica mjini Vatican, eneo ambalo Papa Francis alisimama kwa mara ya kwanza kutoa salamu za pasaka, ndipo hapo ambapo Papa aliombea amani katika bara la Asia, hususan kwa taifa la Korea, kutokana na kuwa katika hatihati ya kuingia vitani baina ya mataifa hayo mawili ya kusini na kaskazini.
"Amani kwa Asia, hasahasa ukanda wa Korea, naomba kutokuelewana kote kugeuke na roho ya mapatano ihuishwe na kuelewana" Papa Francis alianza kuzungumza, akieleza kwa lugha ya Kiitalia, akisalimia watu zaidi ya laki mbili na nusu, katika salamu yake ya pasaka kwa mara ya kwanza akiwa Papa.
Katika salamu hiyo, pia aliomba Yesu awaguse watu wabadili chuki kuwa upendo, kisasi kuwa kusameheana na vita kuwa amani, shirika la habari la Reuters limeripoti.
Ujumbe huu wa Papa umekuja wakati ambao uhusiano wa Korea Kaskazini na Marekani ukiwa katika hali ya mashaka zaidi. Mnamo mwezi uliopita, taifa hilo la Pacific lilisema kuwa linasitisha makubaliano yake ya amaniambayo yalisainiwa mwaka 1953, licha ya kwamba nchi hizo mbili zimekuwa katika hali ya kutaka kupigana kwa kipindi cha miaka 60 sasa.
Viongozi mbalimbali wakisaini mkataba wa makubaliano ya amani baina ya  nchi za Korea.
Korea Kaskazini pia imekuwa ikirusha madongo na kujitamba mbele ya Marekani, ikisema kuwa ina silaha za nyuklia ambazo zina uwezo wa kushambulia mbele ya sheria za Umoja wa Mataifa, katika kujibu hilo, Marekani wao wakatuma nchini Korea Kusini ndege za kivita aina ya F-22, zenye uwezo wa kutoonekana kwenye rada, ili kufanya nao mazoezi ya pamoja na kujiweka tayari kwa chochote ambacho Korea Kaskazini itafanya.

0 comments:

Post a Comment