Monday, March 11, 2013

FILAMU YA "RAY OF HOPE" YA KWAKE PASTOR MYAMBA YACHUKUA TUZO MARA MBILI.

Moja kati ya filamu za Swahiba yangu Pastor Myamba "Ray of Hope" imeweza kujinyakulia tuzo ya "Best Local Language Swahili" kupitia African Magic Viewers Choice Awards.Pastor Myamba amekua ni msani wa kwanza Tanzania kutengeneza filamu za Christian zenye kuonyesha umuhimu wa kumpenda Yesu kristo.

 Katika filamu hiyo waigizaji walio shiriki ni Pastor Myamba,Baby Madaha,Mzee Chilo,na Thea.Muongozaji wa Filamu hiyo Sameer Srivastava na Sajni Sirivastava.Filamu hii ilitengenezwa na kapuni ya Pilipili Entertainment na mwaka jana katika ZIFF ilishinda tuzo ya filamu bora ya Afrika Mashariki.
Kama ujapata copy yako mtu wangu wa karibu itafute ujione.

0 comments:

Post a Comment