Profesa Tibaijuka achangia sh. mil. 46 ujenzi kanisa Katoliki Kitunda
WAZIRI wa Ardhi Nyumba na
Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka amechanga sh. Mil. 46 kwa
ajili ya ujenzi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Kitunda, Jimbo Kuu la Dar
es Salaam.
Profesa Tibaijuka aliyekuwa mgeni
rasmi katika harambee hiyo, Rais wa Awamu ya Tatu, Wiliam Benjamin Mkapa
ambaye hakuwepo katika harambee hiyo alichangia sh. Mil. moja katika ya
sh. mil. 95 zilizochangwa.
Katika harambee hiyo ambayo jiwe la
msingi liliwekwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu...